Uchumi wa kiwango cha chini
Leo katika uchumi tunakuangazia uchumi wa kiwango cha chini kama tulivyoishia wiki lililopita endelea kutufuatilia masomo haya kupitia blogu yetu ya Speak Out With Olais upate kuelewa mambo mbali mbali ya kimaendeleo na nafasi uliyonayo katika kuleta mabadiliko ya kiuchumi katika chi yako....
Karibu ujisomee hapo chini....
Weka poa katika ukurasa wetu wa Facebook leo na uzidi kupata masomo mbalimbali kuhusu maisha ya kijamii kwa ujumla Ingia kiunganishi hiki hapa sasa www.facebook.com/speakoutwitholais
Uchumi wa kiwango cha chini hutazama mwingiliano kupitia masoko
binafsi, huku kukiwa na uhaba na uthibiti wa serikali. Soko linaweza
kuwa la
bidhaa, kama vile mahindi mabichi, au
huduma za kipengele fulani za uzalishaji, kwa mfano upangaji wa matofali. Nadharia hii huzingatia jumla ya kiwango kinachohitajika na wanunuzi na
kiwango kinachohitajika na wanunuzi na
kiwango kinachotolewa
na wauzaji kwa kila bei iwezekanayo kwa kitu kimoja. Inaunganisha mambo
haya pamoja ili kueleza vile soko linaweza kufikia usawazishaji
kulingana na bei na kiwango au kukabiliana na mabadiliko ya soko baada
ya muda.
Huu huitwa kwa kawaida uchambuzi wa ugavi na mahitaji. Miundo ya
soko, kama vile ushindani kamilifu na umiliki, huchunguzwa kwa mtazamo
wa athari kwa tabia na ufanisi wa kiuchumi. Uchambuzi wa mabadiliko
katika soko moja huendelea kutoka kwa fikira ya urahisi kuwa mahusiano
ya tabia katika masoko hubaki bila kubadilika, yaani, uchambuzi wa
sehemu ya usawazishaji. Nadharia ya usawazishaji wa jumla inaruhusu
mabadiliko katika masoko tofauti na ujumla katika masoko yote, zikiwemo
harakati zao na miingiliano yao kuelekea msawazo.|Nadharia ya
usawazishaji wa jumla inaruhusu mabadiliko katika masoko tofauti na
ujumla katika masoko yote, zikiwemo harakati zao na miingiliano yao
kuelekea msawazo.
Masoko
Katika uchumi wa hali ya chini, uzalishaji ni ubadilishaji wa
pembejeo kuwa mazao. Huu ni mchakato wa kiuchumi unaotumia rasilimali
kutengeneza bidhaa ambayo inafaa kubadilishwa. Michakato hii inaweza
kuwa pamoja na utengenezaji, uwekaji kwa bohari, usafirishaji kwa meli,
na kufungasha. Baadhi ya wanauchumi hueleza uzalishaji kwa upana kuwa
shughuli zote za kiuchumi ila tu matumizi. Wao huona kila shughuli ya
uchumi ila ununuzi wa mwisho kama aina ya uzalishaji. Uzalishaji ni
utaratibu, na kwa hivyo hutokea katika wakati na mahali. Kwa sababu ni
dhana ya kufuatana, uzalishaji hupimwa kama “kiwango cha mazao kwa
kipindi cha muda".
Kuna vipengele vitatu katika michakato ya uzalishaji, vikiwemo
kiwango cha bidhaa iliyozalishwa, aina ya bidhaa iliyotengenezwa na
usambazaji wa bidhaa iliyozalishwa kwa mithili ya wakati na mahali.
Gharama ya fursa hutoa pendekezo kuwa kwa kila chaguo, bei ya kweli ya
kiuchumi ni fursa bora zaidi inayofuata. Uchaguzi ni lazima ufanywe
baina ya matendo mawili yanayotamanika lakini ambayo hayawezi
kutekelezwa yote kwa pamoja. Imeelezwa kuwa inayoeleza “uhusiano wa
kimsingi baina ya uhaba na chaguo.". Wazo la gharama ya fursa huwa na jukumu muhimu katika kuhakikisha kuwa rasilimali hutumika kwa ufanisi.
Kwa hivyo, gharama ya fursa haihusu tu gharama za kihazina au kifedha
tu: gharama halisi ya zao la kutotwaliwa, wakati uliopotezwa, radhi au
faida yoyote nyingine ya matumizi inapaswa kuzingatiwa.
Pembejeo na rasilimali zinazotumiwa katika uzalishaji huitwa
vipengele vya uzalishaji. Pembejeo zinazoweza kutumika huwa kwa kawaida
zimewekwa katika makundi sita. Vipengele hivi ni malighafi, mashine,
huduma za kazi, vifaa vya mtaji, ardhi na kampuni. Kwa muda mfupi,
kinyume na muda mrefu, kwa uchache kimoja kati ya vipengele hivi vya
uzalishaji huwa hakibadiliki. Mifano ni pamoja na vifaa, nafasi ya
viwanda inayofaa, na wafanya kazi muhimu.
Kipengele kinachobadilika katika uzalishaji ni kile ambacho kiwango
cha matumizi yake kinaweza kubadilishwa kwa urahisi. Mifano ni pamoja na
matumizi ya nguvu za umeme, huduma za usafirishaji, na nyingi za
pembejeo za malighafi. Katika hali ya “muda mrefu”, vipengele hivi vyote
vya uzalishaji vinaweza kuratibishwa na wasimamizi. Katika hali ya muda
mfupi, “kadiri ya utendakazi” ya kampuni huamua idadi ya juu zaidi cha
mazao ambao yanaweza kuzalishwa, lakini katika hali ya muda mrefu,
hakuna mpaka wa idadi. Mabadiliko ya jail ya muda mrefu na muda mfupi
huwa na nafasi muhimu katika miundo ya kiuchumi.
Ufanisi wa kiuchumi hueleza ni vipi mfumo unaweza kuzalisha mazao ya
kiwango cha juu zaidi yanayohitajika kwa kutumia utaratibu fulani wa
pembejeo na teknolojia iliyoko. Ufanisi huboreshwa ikiwa mazao mengi
yanazaliswa pasi na kubadili pembejeo, au kwa usemi mwingine, kiwango
cha “msuguano” au “upotevu” kinapunguzwa. Wanauchumi hutafuta ufanisi wa
Pareto, ambao hufikiwa pale mabadiliko hayawezi kumfaidi mtu bila
kumdhuru mtu mwingine.
Ufanisi wa kiuchumi hutumika kuashiria idadi ya dhana ambazo
zinahusiana. Mfumo unaweza kusemwa kuwa na ufanisi wa kiuchumi iwapo:
hakuna atakayefaidika bila kumdhuru mwingine, mazao mengi zaidi hayawezi
kupatikana bila kuongeza kiwango cha pembejeo, na uzalishaji
huhakikisha gharama ya chini zaidi iwezekanavyo kwa kitengo. Fafanuzi
hizi za ufanisi hazina maana inayofanana barabara. Hata hivyo,
zimezungukwa zote na dhana kuwa hakuna kitu zaidi kinachoweza kupatikana
kwa kutumia rasilimali zilizoko.
Umaalumu
Umaalumu huchukuliwa kuwa kipengele muhimu kwa ufanisi wa kiuchumi
kwa sababu watu au nchi tofauti huwa na manufaa linganifu. Huku nchi
moja inaweza kuwa na manufaa kamili katika sehemu zote juu ya nchi
zingine, inaweza hata hivyo kuwa na umaalumu katika sehemu ambayo kwa
kiwango fulani ina manufaa linganifu, na hivyo kufaidikika kwa kufanya
biashara na nchi ambazo hazina manufaa kamili. Kwa mfano, nchi inaweza
kuwa na umaalumu katika uzalishaji wa bidhaa za kiteknolojia za hali ya
juu, kama vile nchi zilizostawi hufanya, na kufanya biashara na mataifa
yanayostawi kwa bidhaa zinazozalishwa katika viwanda, ambapo wafanyakazi
hupatikana kwa bei rahisi na kwa wingi.
Kwa mujibu wa nadharia, katika njia hii bidhaa jumla na utumizi zaidi
vinaweza kupatikana kuliko ikiwa nchi zinazalisha bidhaa zao zenyewe za
kiwango cha juu na zile za kiwango cha chini. Nadharia ya manufaa
linganifu huwa san asana ndiyo kigezo cha imani ya mwanauchumi wa
kawaida katika faida ya biashara huru. Dhana hii huhusisha watu binafsi,
mashamba, watengenezaji, watoaji wa huduma, na chumi. Baina kila
mojawapo ya mifumo hii ya uzalishaji, kuna uwezekano wa kuwa na
ugavi wa ajira
unaohusiana ambapo kila mfanyakazi huwa na kazi tofauti au hufanya kazi
maalumu kama sehemu ya juhudi za uzalishaji, au kwa uhusiano aina
tofauti za vifaa vya mtaji na matumizi tofauti ya ardhi.
Kitabu cha Wealth of Nations (1776) cha Adam Smith huzungumzia faida
za ugavi wa ajira. Smith alinena kuwa mtu anafaa kuwekeza rasilimali,
kwa mfano, ardhi au kazi, ili kuchuma mapato ya juu yawezekanayo
kutokana na uwekezaji huo. Hivyo, matumizi yote ya rasilimali yanafaa
kuzalisha kiwango sawa cha mapato (ambacho kimeratibishwa na athari za
kila biashara). La sivyo ubadilishaji hutokea. Wazo hili, aliandika
George Stigler, ndilo shauri kuu la dhana ya kiuchumi, na kwa sasa
huitwa nadharia ya pembezoni ya uzalishaji ya ugavi wa mapato.
Mwanauchumi wa Kifaransa Turgot alikuwa amelizungumzia swala hilo hilo
mnamo 1766.
Katika maneno ya kawaida zaidi, kuna nadharia kuwa motisha za soko,
ikiwemo bei ya mazao na pembejeo za uzalishaji, huchagua mgawo wa
vipengele vya uzalishaji kwa
manufaa linganifu , yaani, ili kwamba pembejeo za bei ya chini (kwa kiwango fulani) zinatumika ili kumudu chini
gharama ya fursa ya aina fulani ya mazao. Katika mchakato huu, jumla ya mazao huongezeka kama matokeo ya kutopanga au kwa kukusudia.
Umaalumu kama huo wa uzalishaji hubuni fursa kwa faida kutoka kwa
biashara ambapo wenye rasilimali hufaidika kwa biashara kutokana na
uuzaji wa aina moja ya mazao kwa bidhaa zingine, zilizo na thamani kubwa
zaidi. Kipimo cha faida kutokana na biashara
ni ongezeko la mazao (rasmi, jumla ya ongezeko la
mabaki ya mtumiaji na faida za mzalishaji) kutoka kwa umaalumu wa uzalishaji na biashara inayofuatia.
Ugavi na mahitaji
alt = A depicting Quantity graph ya X-axis na Price juu ya Y-axis
Nadharia ya mahitaji na ugavi ni kanuni andalizi ya kueleza bei na
viwango vya bidhaa ambavyo vimeuzwa na mabadiliko yanayofuatia katika
uchumi wa soko. Katika nadharia ya uchumi wa kiwango cha chini,
huashiria uamuzi wa bei na mazao katika soko lililo na ushindani kamili.
Hii imekuwa ni kigezo muhimu kwa uundaji wa mifumo mingine ya masoko na
kwa mielekeo mingine ya kinadharia.
Kwa soko fulani ya bidhaa, mahitaji huonyesha kiwango ambacho
wanunuzi wanaotazamiwa watakuwa tayari kununua kwa kila kitengo cha
bidhaa. Mahitaji mara nyingi huonyeshwa kwa kutumia jedwali au mchoro
unaohusisha bei na kiwango kinachohitajika (tazama mchoro ulio katika
kijisanduku). Nadharia ya mahitaji hueleza wanunuzi wa kibinafsi kama
ambao huchagua kwa kufikiria kiwango ambacho kinatamanika cha kila
bidhaa, kulingana na mapato, bei, mapendeleo, na kadhalika. Maneno
yanayotumika kuelezea hali hii ni ‘utumiaji uliozuiwa wa hali ya juu’
(huku mapato yakiwa ndiyo kizuizi kwa mahitaji). Hapa, utumiaji
huashiria (kwa makisio) mapendeleo ya watumiaji wa kibinafsi. Utumiaji
na mapato hutumiwa basi kubuni mali ya kukisia kuhusu athari ya
mabadiliko ya bei kwa kiwango kinachohitajika.
Sheria ya mahitaji husema kuwa, kwa ujumla, bei na kiwango
kinachohitajika katika soko fulani huhusiana kwa kinyume. Yaani, ikiwa
bei ya bidhaa ni ya juu, basi watu wachache zaidi huwa na uwezo au
utashi wa kuinunua (ikiwa vitu vingine havibadiliki). Jinsi bei ya
bidhaa inavyoongezeka, ndivyo uwezo wa kununua hupungua (matokeo ya
mapato) na watumiaji huelekea katika bidhaa zenye bei ya chini zaidi
(matokeo ya ubadala). Vipengele vingine vinaweza pia kuathiri mahitaji;
kwa mfano kuongezeka kwa mapato kutasogeza mchirizo wa mahitaji kuelekea
upande wa nje kulingana na chanzo, ilivyo katika mchoro.
Ugavi ni uhusiano baina ya bei ya bidhaa ya kiwango kilichopo kwa
kuuza kutoka kwa wasambazaji (kama vile wazalishaji) katika bei hiyo.
Ugavi mara nyingi huelezwa kwa kutumia jedwali au mchoro unaohusisha bei
na kiwango kinachosambazwa. Wazalishaji wanakisiwa kuwa wanaotaka
kuzalisha faida ya kiwango cha juu zaidi, kumaanisha wanajaribu
kuzalisha kiwango cha bidhaa ambacho kitawaletea faida ya juu zaidi.
Ugavi kwa kawaida huashiriwa kama uhusiano wa moja kwa moja baina ya bei
na kiwango kilichosambazwa (ikiwa vitu vingine havibadiliki).
Hivi ni kusema kuwa, ikiwa bei ambayo bidhaa inaweza kuuzwa ni ya
juu, basi wengi wa wazalishaji wataisambaza. Bei hii ya juu zaidi
hufaidisha kuongezeka kwa uzalishaji. Katika bei iliyo chini ya msawazo,
kuna uhaba wa kiwango kinachosambazwa ikilinganishwa na kiwango
kinachohitajika. Hii inasogeza bei chini. Muundo wa ugavi na mahitaji
hutabiri kuwa kwa kila mchirizo wa ugavi na mahitaji, bei na kiwango
vitaimarika kwa bei ambayo itafanya kiwango kinachosambazwa kuwa sawa na
kiwango kinachohitajika. Hii inasogeza bei chini. [[]]Muundo wa ugavi
na mahitaji hutabiri kuwa kwa kila mchirizo wa ugavi na mahitaji, bei na
kiwango vitaimarika kwa bei ambayo itafanya kiwango kinachosambazwa
kuwa sawa na kiwango kinachohitajika. Hii ni katika mkingamo wa
michirizo miwili katika mchoro ulio hapa juu, msawazo wa soko.
Kwa kiwango fulani cha bidhaa, mahali halisi pa bei katika mchirizo
wa mahitaji huonyesha thamani, au utumiaji wa pembezoni kwa watumiaji
kwa kitengo hicho cha cha mazao. Inapima bei ambayo mtumiaji anaweza
kuwa tayari kulingana na kitengo cha bidhaa. Mahali halisi pa bei katika
mchirizo wa ugavi hupima gharama ya pembezoni, ongezeko la gharama ya
jumla kwa msambazaji kulingana na kitengo cha bidhaa. Bei katika msawazo
huamuliwa na ugavi na mahitaji. Katika soko lililo na ushindani halisi,
ugavi na mahitaji hulinganisha gharama na thamani katika
msawazo.|Katika soko lililo na ushindani halisi, ugavi na mahitaji
hulinganisha gharama na thamani katika msawazo.
Mahitaji na ugavi vinaweza pia kutumika kulinganisha usambazaji wa
mapato kwa vipengele vya uzalishaji, vikiwemo kazi na mtaji, kupitia
masoko husika. Katika soko la wafanyakazi, kwa mfano, idadi ya
wafanyakazi walioajiriwa na bei ya kuwalipa (kiwango cha marupurupu)
huonyeshwa kama yaliyowekwa na mahitaji ya kupata wafanyakazi (mahitaji
ya makampuni ya biashara na kadhalika kwa uzalishaji) na utoaji wa
ufanyakazi (kutokwa kwa wafanyakazi).
Mahitaji na ugavi hutumika kueleza tabia ya soko lililo na ushindani
kamili. Mahitaji na ugavi vinaweza kujumuishwa ili kueleza vigezo
vinavyobadilika katika uchumi woue, kwa mfano, kiwango cha mazao yote na
hali ya kawaida ya bei, vinavyotafitiwa katika somo la uchumi wa
kiwango cha juu.
Katika uchambuzi wa ugavi na mahitaji, bei ya bidhaa huratibu viwango
vya uzalishaji na utumiaji. Bei na kiwango vimeelezwa kama jinsi
zinazoonekana zaidi moja kwa moja katika bidhaa iliyozalishwa kwa
soko.|Bei na kiwango vimeelezwa kama jinsi zinazoonekana zaidi moja kwa
moja katika bidhaa iliyozalishwa kwa soko.
Ugavi, mahitaji na msawazo wa soko ni vigezo vya kinadharia
vinavyounganisha bei na kiwango. Lakini kufuatilia athari za vipengele
vinavyotabiriwa kugeuza ugavi na mahitaji – na kupitia kwao, bei na
kiwango – ni zoezi la kawaida katika masomo tendaji ya uchumi wa kiwango
cha chini na uchumi wa kiwango cha juu. Nadharia ya uchumi inaweza
kubainisha ni katika mazingira yapi bei huwa kifaa mwafaka cha
mawasiliano cha kuratibu kiwango.
Utumiaji katika hali halisi duniani unaweza kujaribu kupima ni kwa
kiwango kipi vigezo vinavyobadilika na vinavyoongeza ugavi na mahitaji
hubadilisha bei na kiwango.
Upembezoni ni matumizi ya dhana za pembezoni katika somo la kiuchumi.
Dhana za pembezoni huhusishwa na badiliko fulani katika kiwango
kilichotumika cha bidhaa au huduma, na wala si wazo la umuhimu unaopita
kiasi wa hiyo aina ya bidhaa au huduma, au wa ujumla wa aina yoyote ile.
Dhana kuu ya upembezoni halisi ni ile ya utumiaji wa pembezoni, lakini
wasomi wa dhana hii waliofuata mwongozo wa Alfred Marshall walizidi
kutegemea sana dhana ya uzalishaji wa unaoonekana wa pembezoni katika
maelezo yao ya bei; na mapokeo ya urasimimpya ambao yalitokana na
upembezoni wa Uingereza yaliasi dhana ya utumiaji na kuyapa mabadiliko
ya viwango vya pembezoni umuhimu zaidi katika uchambuzi wao.
Kuanguka kwa soko
alt = A smokestack ikitoa moshi
Maneno “kuanguka kwa soko” hujumuisha matatizo kadha wa kadha ambayo
hudhoofisha fikira za kawaida za kiuchumi. Ingawa wanauchumi huorodhesha
kuanguka kwa soko katika makundi tofauti, makundi yafuatayo hupatikana kutokana na nakala kuu.
Makundi asili yanayotawala shughuli za soko, au dhana zinazoambatana
za kundi tawala “tendaji” au “la ustadi”, huhusisha ulegevu wa ushindani
katika kuthibiti wazalishaji. Tatizo hili huelezwa kama hali ambapo
ikiwa bidhaa itaendelea kuzalishwa zaidi, basi mapato yanakuwa ya
kiwango cha juu. Hii humaanishwa kuwa hali hii humfaidi tu mzalishaji
mmoja.
Kutolingana kwa habari hutokea pale kikundi kimoja kina maelezo zaidi
au bora zaidi kuliko kingine. Kuwepo kwa kutolingana kwa habari huzua
matatizo kama shida za kimaadili, na uteuzi mbaya, ambayo hutafitiwa
katika nadharia ya mkataba. Uchumi wa habari hufungamana na maswala
mengi, ambayo ni pamoja na fedha, bima na sheria ya mkataba, na maamuzi
chini ya hali za hatari na ukosefu wa uhakika.
Masoko yasiyokamilika ni jina ambalo hutumika katika hali ambapo
wanunuzi na wauzi hawana habari ya kutosha kuhusu hali ya mwingine
ilikuweza kuweka bei ya bidhaa au kutoa huduma ipasavyo. Huku kikitokana
na makala ya George Akerlof ya Market for Lemons, kiolezo cha kutoa
mfano ni kile cha soko yenye hila ya magari yaliyotumika. Wateja
wasiokuwa na uwezo wa kujua iwapo wananunua “limau” watasukuma bei ya
wastani chini zaidi kuliko ile bei inayostahili kwa ya gari nzuri
iliyotumika. Kwa njia hii, bei inaweza kutoonyesha thamani ya kweli.
Bidhaa za umma ni bidhaa ambazo zina uhaba katika soko la kawaida.
Jinsi za kutambua hali hii ni kuwa watu wanaweza kutumia bidhaa hizi
pasi na kuzilipia na kuwa zaidi ya mtu mmoja anaweza kutumia bidhaa hii
kwa wakati mmoja.
Vipengele vya nje huzuka pale ambapo kuna gharama au faida za juu za
kijamii kutoka kwa uzalishaji au utumiaji ambavyo havidhihiriki katika
bei za soko. Kwa mfano, uchafuzi wa hewa unaweza kuzua kipengele cha nje
kisichofaa, na elimu inaweza kuzua kipengele cha nje kilicho na manufaa
(kupungua kwa uhalifu, na kadhalika.). Serikali mara nyingi hulipisha
kodi kwa na kuweka vizuizi kwa bidhaa zilizo na vepengele vya nje
visivyofaa katika jitihada za kurekebisha upotovu wa bei unaosababishwa
na vipengel hivi vya nje.
Nadharia ya kimsingi ya mahitaji-na-ugavi hutabiri msawazo lakini si
kasi ya urekebishaji wa mabadiliko ya msawazo kutokana na mabadiliko
katika mahitaji na ugavi.
Katika sehemu nyingi, aina fulani ya utobadilikaji wa bei hukubalika
ili kueleza sababu ya viwango, na wala si bei, na kurekebisha kwa muda
mfupi mabadiliko katika upande wa mahitaji au ule wa ugavi. Hii
hujumuisha uchambuzi wa kawaida wa maisha ya biashara katika somo la
uchumi wa kiwango cha juu. Uchambuzi mara nyingi huhusisha sababu za
kutobadilika huku kwa bei na athari zake katika kufikia msawazo
unaokisiwa kwa muda mrefu. Mifano ya kutobadilika kwa bei katika masoko
fulani ni pamoja na viwango vya marupurupu katika soko la ajira na bei
zilizowekwa katika masoko ambayo hayana ushindani kamili.
Ukosefu wa kuimarika kwa uchumi wa kiwango cha juu, unaozungumziwa
hapa chini, ni chanzo muhimu cha kuanguka kwa soko, ambapo kupotea kwa
uthabiti wa biashara kwa ujumla au mshtuko wan je unaweza kusitisha
uzalishaji na usambazaji, na hivyo kudhoofisha masoko ambayo yalikuwa
yameimarika hapo awali.
Baadhi ya masomo yaliyochanganuliwa ya kiuchumi hushughulika na kuanguka
kwa masoko kuliko mengine. Uchumi wa sekta ya umma ni mfano mmoja,
kwani iwapo masoko huanguka, basi aina fulani ya uthibiti au mpango wa
serikali ndilo jibu. Nyingi za chumi za kimazingira huhusisha
vipengele vya nje au “mabaya ya umma".
Aina za sera hujumuisha vithibiti ambavyo huonyesha uchambuzi wa
gharama-faida au ufumbuzi wa masoko ambao hubadili motisha, kama vile
ada za uchafuzi wa mazingira au udhihirishaji upya wa haki za kumiliki
mali.
Makampuni
alt = watu wawili kukaa saa kompyuta wachunguzi na taarifa ya fedha
Mojawapo ya fikira kuhusu masoko yaliyo na ushindani kamili ni kuwa
kunao wazalishaji wengi, hamna baina yao anayeweza kushawishi mabadiliko
ya bei wala kufanya kazi pasi na kuzingatia masharti ya soko. Hata
hivyo, katika hali halisi, watu hawafanyi biashara tu kwa soko, huwa
wanafanya kazi na kuzalisha katika makampuni. Aina za wazi kabisa za
makampuni ni mashirika, ubia na amana. Kwa mujibu wa Ronald Coase, watu
huanza kupanga uzalishaji wao katika makampuni wakati gharama za kufanya
biashara huwa za chini kuliko wakati wafanyapo shughuli hizi sokoni.
Makampuni hujumuisha kazi na mtaji, na zinaweza kupata faida nyingi
zaidi za upanuzi ( wakati kuzalisha vitu viwili zaidi ni nafuu zaidi
kuliko kuzalisha kitu kimoja) kuliko kufanya biashara ya kitu kimoja
katika soko.
Uchumi wa ajira hutafuta kuelewa utendakazi wa soko na mienendo ya
ajira. Masoko ya ajira hufanya kazi kupitia kwa mwingiliano wa
wafanyakazi na waajiri. Uchumi wa ajira huangalia watoaji wa huduma za
kazi (wafanyakazi), wanaohitaji huduma za kazi (waajiri), na juhudi za
kuelewa mifumo inayotokea ya marupurupu na mapato mengine kutokana na
kazi na ya ajira na ukosefu wa ajira. Matumizi halisi ni pamoja na
kusaidia katika ubuni wa utumizi kamili wa sera.
Mpagilio wa viwanda hutafiti tabia za mikakati ya makampuni, miundo
ya soko na maingiliano yao. Miundo ya kawaida ya masoko iliyotafitiwa ni
pamoja na ushindani kamili, ushindani ulio na kundi moja lililo na
sehemu kubwa ya shughuli za sokp, na aina nyingi ya makundi kadhaa
yanayomiliki sehemu kubwa ya soko, na kundi moja linalomiliki sehemu
kubwa ya soko.
Uchumi wa kifedha, huitwao mara nyingi fedha, hushughulika na ugavi
wa rasilimali za kifedha katika mazingira ambayo hayana uhakika (au
yaliyo na hatari fulani). Kwa hivyo, zingatio lake ni katika utendakazi
wa masoko ya kifedha, uwekaji wa gharama katika vifaa vya kiuchumi, na
miundo ya kifedha ya makampuni.
Uchumi wa usimamizi hulinganisha uchambuzi wa uchumi wa kiwango cha
chini na maamuzi maalumu katika makampuni ya biashara au vitengo vya
usimamizi. Uchumi huu hutegemea sana sana na mbinu za kujumuisha wingi
kama vile utafiti wa utendakazi na utaratibishaji na kutoka kwa mbinu za
takwimu kama vile uchambuzi wa kuridi nyuma katika hali ya ukosefu wa
uhakika na habari kamilifu. Hoja ya kuunganisha ni jaribio la kuimarisha
ufanisi wa maamuzi ya kibiashara, ikiwemo kupunguza iwezekanavyo kwa
bei ya kitengo na kuongeza iwezekanavyo kwa faida, kulingana na malengo
ya kampuni na vikwazo vinavyotokana na teknolojia na hali ya soko.
Sekta ya umma
Fedha za umma ni sehemu ya uchumi ambayo hushughulika na ubuni wa
bajeti ya mapato na matumizi ya kitengo cha sekta ya umma, kwa kawaida
serikali. Mada hii hushughulikia maswala kama vile malipo ya ushuru (ni
nani hasa analipa ushuru fulani), uchambuzi wa gharama-faida wa mipango
ya serikali, athari juu ya ufanisi wa kiuchumi na ugavi wa mapato katika
aina tofauti za matumizi na ushuru, na siasa za kifedha. Jambo hili la
mwisho, ambalo ni kipengele cha nadharia ya chaguo ya umma, hubuni tabia
ya sekta ya umma kama mfano wa uchumi wa kiwango cha chini, unaohusisha
maingiliano ya wapiga kura wanaojali maslahi yao wenyewe, wanasiasa, na
wafanyakazi wa serikali au mashirika mengine.
Wingi wa uchumi ni wa manufaa, kwani hutafuta kueleza na kutabiri
matukio ya kiuchumi. Uchumi wa kuamua thamani (normative economics)
hujihusisha na kubaini lililo zuri au baya kiuchumi.
Uchumi wa ustawi ni tawi la uchumi wa kuamua thamani unaotumia ustadi
wa uchumi wa kiwango cha chini ili kubainisha kwa wakati huo huo
ufanisi wa ugavi katika uchumi na ugavi wa mapato unaohusishwa nao. Huwa
unajaribu kupima ustawi wa jamii kwa kuchunguza shughuli za kiuchumi za
watu wanaobuni jamii.
Imeandaliwa na Mtangazaji wako Olais kwa ushirika wa Wikipedia