Advertise with us today here...

Reach your market today and expand your network and increase your profit....

Advertise with us today contact us via marketing@olais.co.tz | +255757599666

Vitenge Market

Vitenge Market
Vitenge market place offers you the best and quality vitenge just contact us today

SOWO - Online Market

SOWO - Online Market
Get new and used products online by visit our site everyday hit the link and get subscribed

Tuesday, 18 November 2014

Bi harusi apewa talaka siku ya harusi


Bi harusi apewa talaka siku ya harusi.Picha niaba ya gazeti la Daily Mirror nchini Uingereza

Bwana harusi mmoja kutoka Saudi Arabia amempa talaka mkewe siku ya harusi baada ya kumuona uso wake kwa mara ya kwanza wakati mpiga picha alipotaka kuwapiga picha.
Maharusi hao kutoka mji wa magharibi wa Saudia,Medinah walikubaliana kuoana licha ya kutoonana uso kwa uso,swala ambalo ni utamaduni mkubwa wa mataifa ya mashariki ya kati.
lakini wakati mwanamke huyo alipofungua kitambara alichokuwa amejifunika uso na kutabasamu katika kamera,mumewe alishtuka na kuondoka wa ghafla.
Kulingana na gazeti moja katika eneo hilo kwa jina Okaz,mwanamume huyo alianguka na kuzirai huku wageni waalikwa wakijaribu kuingilia kati ili kutatua kilichokuwa kikiendelea.
Hatahivyo Bwana harusi alisema kuwa hakuweza kumwona bi harusi kabla ya harusi yao gazeti hilo la Okaz liliripoti.
'' Si wewe msichana niliyetaka kuoa,si wewe kamwe niliyedhani '' kwa hivyo nakupa talaka''alisema bwana harusi.
Na alipompa talaka bi harusi naye alianguka na kuzirai na kuifanya harusi hiyo kuwa usiku wa majonzi.

Chanzo: BBC Swahili

Bikira, kigezo kuwa Polisi Indonesia

Soma habari kamili...

Polisi wa kike waelezwa kudhalilishwa kufanyiwa kipimo cha bikira
Serikali ya Indonesia inaelezwa kuruhusu kuwafanyia wanawake wanaotaka kujiunga na Jeshi la Polisi kipimo cha bikira ,shirika la Human rights Watch limeeleza.
Shirika hilo uangalizi wa haki za binaadam liliwahoji Polisi wanawake na wanaotaka kujiunga na Jeshi la polisi ambao tayari wamepimwa katika miji sita ya nchini Indonesia,wawili kati yao wamefanyiwa kipimo hicho mwaka huu.
Kipimo cha bikira kimeorodheshwa kuwa moja ya matakwa ya kuingia kwenye Jeshi, tovuti ya polisi imeeleza.
Wanawake waliofanyiwa kipimo hicho wamesema walipata maumivu na kujisikia kudhalilishwa.
Askari wa kike walishapeleka malalamiko kwa ngazi za juu za jeshi la Polisi bila mafanikio.
Afisa wa juu wa Human Rights Watch,Nisha Varia amesema kipimo hicho ni unyanyasaji na kinawadhalilisha wanawake, amewataka polisi mjini Jakarta kufuta kipimo hicho na kukipiga marufuku nchi nzima.
Polisi nao wanasema kuwa hawafanyi kipimo hicho kwa sasa kwa kuwa wamepiga marufuku.
Hata hivyo hakuna ushahidi wa kutosha kuwa Jeshi la Polisi limesitisha kitendo hicho kwa kuwa katika tovuti yake eneo la kazi tangazo la tarehe 5 mwezi Novemba mwaka 2014 imeeleza kuwa wanawake wanaotaka kuwa polisi wanapaswa kujaribiwa kama wana bikira,hivyo basi wanawake wanaotaka kuwa askari wanapaswa kutunza bikira zao.Wanawake walioolewa hawapewi nafasi hiyo.
Mashuhuda wanasema kuwa jaribio la bikira hufanywa katika hospitali zinazoendeshwa na jeshi la Polisi, vidole hutumika katika kubaini kama mwanamke ni bikira au la.
Shirika la Human Rights Watch limesema kipimo hiki hufanywa na Polisi pia nchini Misri, India na Afghanistan.
Mwaka 2010 Brigedia Jenerali, Sigit Sudarmanto alieleza namna alivyotofautiana na wenzake kuhusu kipimo cha bikira kwa wanawake yeye haungi mkono.
Kisa cha kufanywa kwa kipimo hiki dhidi ya wanawake ni madai kuwa hawahitaji wanawake wasio bikira wakiwafananisha na makahaba.
Lakini swali linabaki kuwa je kuna ushahidi wa kisayansi kuwa aliye bikira hufanya kazi kwa ufanisi zaidi kuliko asiye bikira, je asiye na bikira hana adabu kuliko aliye nayo?
Sudarmanto amesema baada ya kulumbana kwa muda mrefu iliridhiwa kusitishwa kwa zoezi hilo, hata hivyo inashangaza kuona bado hali ni ileile japo ahadi ya kusitishwa ilitolewa.

Chanzo: BBC Swahili