Advertise with us today here...

Reach your market today and expand your network and increase your profit....

Advertise with us today contact us via marketing@olais.co.tz | +255757599666

Vitenge Market

Vitenge Market
Vitenge market place offers you the best and quality vitenge just contact us today

SOWO - Online Market

SOWO - Online Market
Get new and used products online by visit our site everyday hit the link and get subscribed

Tuesday, 21 October 2014

Pinda atangaza nia ya kugombea uraisi 2015 kimya kimya.

Mh. Mizengo Pinda akiwa katika studio za BBC- Swahili hapa
mjini Uingereza katika mahojiano na mtangazaji Salim Kikeke
(Picha na BBC - Swahili)
Mh. Mizengo K. Pinda akiwa katika mahojiano na Mtangazaji Salim Kikeke wa BBC - Swahili katika studio za hapa mjini Uingereza. Mh. Pinda alitamka kwa kuficha pasipo kuweka wazi maneno ya kuthibitisha kuwa atakuwa miongoni mwa wagombea wa kiti cha uraisi wa nchi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwa kama atakuwa miongoni mwa watakaokuwa katika mchakato huo na kufanikiwa kupitishwa na halmashauri kuu ya chama chake basi atakuwa ni mgombea wa kiti cha uraisi kwa mwaka 2015.
Swali hili limekuwa gumu kwa Mh. Pinda kulijibu ikiwa ni hasa bado kiongozi wa serikali. Ndugu Salim Kikeke aliuliza swali hili akiwa na lengo la kutaka kujua kuwa mchakato wa katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania umefikiwa wapi watu wakiwa wanasema ya kuwa katiba hii ni ya chama kimoja yaani chama tawala?

Huku Mh. Pinda akijibu swali hili alitoa ufafanuzi mzuri ikiwa ni kwamba katiba ya tume ilipelekwa ndani ya Bunge Maalum la katiba kwa lengo la maboresho na sio kwa lengo la kuipitisha katiba.

Ni jibu zuri na tukumbuke ya kuwa ndio kazi nchi iliyowatuma wabunge hawa kwenda kuifanya na ndio maana kuna kazi mamia zimekwama ikiwa ni lengo la kuhakikisha ya kuwa nchi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tunakuwa na katiba bora na yenye maslahi kwa taifa letu la leo na kesho na kwa vizazi vyote.

Ingia link hii hapa ujionee na kusikia kipande kidogo cha Mh. Pinda kutangaza nia akiwa katika mahojiano na Ndugu. Kikeke katika studio za BBC - Swahili hapa mjini Uingereza.

https://www.facebook.com/video.php?v=509239709213496&set=vb.174247279379409&type=2&theater

Mwandishi wako Olais K. Raphael | Speak Out With Olais - Media

No comments:

Post a Comment